Tuesday, October 2, 2012

MOURINHO: NITARUDI UINGEREZA KUFUNDISHA

Kocha wa Real Madrid Jose Mourinho
Kocha wa Real Madrid Jose Mourinho amesema atarudi kufundisha soka la nchini Uingereza wakati atakapomaliza mkataba wake na Real Madrid lakini mreno huyo amesema kuwa ana furaha kuwepo Bernabeu.

Wakati kocha huyo wa zamani wa Chelsea akiwa na mkataba na Real Madrid hadi 2016, anadhani kuwa kazi yake ijayo itakuwa ni kurejea katika ligi kuu ya Premier.
''Nimesema wazi kuwa, kwa sababu nyingi, baada ya hili hatua ijayo itakuwa ni Uingereza'' Mourinho mwenye miaka 46 aliiambia CNN.

''Ni lini? sijui, sifahamu.Nina furaha kwa wakati huu kuwa meneja wa klabu bora duniani''.
Mourinho alijiunga Real Madrid akitokea Inter Milan mwaka 2010 baada ya kuipa taji la tatu la Ligi Klabu Bingwa Ulaya timu hiyo ya Italia

No comments:

Post a Comment