Tuesday, October 2, 2012

JOSE MOURINHO: NAYACHUKIA MAISHA YANGU YA KIJAMII..WATU SASA WANANIDHIHAKI




Kocha wa Real Madrid Jose Mourinho amesema kuwa umaarufu na kujulikana kunakokuja kupitia kufundisha soka ni mgumu sana kuubeba.
Meneja huyo wa Real Madrid akiongea na CNN,alisema mtoto wake mwenye umri wa miaka 12 amekashifiwa na hiyo inafanya kuwa ngumu kuishi maisha ya kawaida.
"Kama ningeweza kuwa kocha, kocha wa soka, kwa muda huu nikaondoka klabuni baada ya mechi na kuzima mwanga wote na kuwa mtu mpya ambaye hakuna mtu anayemjua, nigefanya kazi hiyo vizuri kwa raha," aliambia CNN.

"Kwasababu nayachukia maisha yangu ya kawaida. Sipendi maisha ya ustaa. Nachukizwa sana na kushindwa kuishi maisha ya kawaida, kama baba ambaye anaenda na mwanae wa kiume kuangalia soka na kuwa pale na wababa wengine 20 tunaangalia mchezo huo.

"Nipo kwenye mechi ya soka ya watoto wa miaka 10-12 na ninatakiwa kuwepo pale, watu wanakuja na kuanza kuomba kupiga nao picha, washabiki wanakuja kwa kutaka kupata saini,Wengine wanakuja kunitukana tu, wengine huenda golini kwenye lango analodaka mwanangu mwenye miaka 12 na kumtukana mwanangu."  
Source:The Independent

No comments:

Post a Comment