Tuesday, October 2, 2012

ZLATAN IBROHIMOVICH: MESSI HASTAHILI KUWA MCHEZAJI BORA WA DUNIA KWA MAKA HUU

Ibrahimovich akimtazama Messi enzi hizo wakiwa wote Barcelona

Ibrahimovich akifurahia ushindi pamoja na Messi enzi hizo wakiwa wote Barcelona
Mchezaji wa zamani wa Barcelona na Intermilan Zlatan Ibrahimovich amefunguka na kusema kuwa mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi hastahili kushinda tuzo ya mwanasoka bora wa dunia mwaka huu kwa sababu msimu uliopita ameshinda kikombe kimoja tu kidogo, mchezaji mwenzake wa zamani wa Barcelona Zlatan Ibrahimovic amesema leo Jumanne.

"Messi amekuwa na msimu mzuri binafsi lakini hajashinda kitu chochote kikubwa na tayari ameshashinda Ballon d'Or mara 3," Mshambuliaji wa Pars Saint Germain Ibrahimovic, ambaye alicheza na Messi katika msimu wa 2009/10, aliiambia Eurosport jumanne hii.


"Inategemea aidha unampa mtu zawadi kwa kazi yake binafsi ay yenye mkusanyiko. Xavi bado anacheza katika kiwango cha juu, Iniesta pia alikuwa na msimu mzuri, wameshinda Euro wakati Messi ameshinda kikombe kidogo cha mfalme . Messi ameshahsinda Ballon D'Or mara 3 nafikiri msimu huu hastahili na muda huu nafikiri ni sahihi akishinda mtu mwingine."


Tuzo ya Ballon d'Or  itatolewa mwezi January tarehe 7 mwakani.

No comments:

Post a Comment